|  | 
| Chuchu Hans | 
RJ Company chini ya Blandina Chagula(Johari) na Vicent Kigosi(Ray) 
wanakuja na filamu mpya ya Love Maniac na hii ni exclusive news ambayo Blog ya swahili planet
 imeipata kutoka kwa chanzo makini kilicho karibu na watengenezaji wa 
filamu hiyo. 
|  | 
| Muonekano wa Ray katika filamu ya Love Maniac...... | 
Kama hivi karibuni umeona Ray akiwa na tattoo nyingi 
mwilini na nywele za blond basi ni kwa ajili ya character yake katika 
filamu hii ambapo amecheza kama kijana wa kisasa na mhuni. Muigizaji 
mkuu wa kike wa filamu hii ni Chuchu Hans ambaye anapendwa sana 
kimapenzi na kijana mstaarabu ambapo nafasi hiyo imechezwa na Walter De 
Ngonde lakini Chuchu hapendi wanaume na hamtaki kabisa Walter ambaye 
anafikia hatua anawatumia wazazi wake(Mzee Masinde) wamsaidie kumpata 
Chuchu lakini mwishowe Chuchu anaangukia kimapenzi kwa kijana mhuni 
mwenye tattoo nyingi mwilini ambapo nafasi hiyo imechezwa na na Ray na 
hatimaye Chuchu anakuwa kichaaa kutokana na issues za mapenzi. Mastaa 
wengine katika filamu hiyo ambayo bado inashutiwa kwasasa ni Kupa.
 
 
No comments:
Post a Comment