Msanii wa filamu za Kibongo, Jumanne Mshindo anadaiwa kumfanyia fujo 
mama mwenye nyumba wake, Farida Hamisi kisha kutuhumiwa kumpiga na 
kumjeruhi huku akijua ana mimba.
 
 
Msanii wa filamu Bongo, Jumanne Mshindo.
Akizungumza na namba moja la mastaa na skendo za kijamii,  hivi karibuni, Mbagala jijini Dar, Farida alisema kuwa 
kisa cha kupigwa ni rafiki yake ambaye alipeleka maneno kwa mke wa 
msanii huyo.
“Unajua Jumanne alikuwa akinitaka nikamkataa na kumwambia mume wangu 
ambaye aliniambia nimdharau kwa sababu ya tamaa zake, sikuishia hapo 
nilimueleza rafiki yangu mmoja ambaye alipeleka maneno kama yalivyo kwa 
mke wa Jumanne,” alisema Farida.
Mama mwenye nyumba, Farida Hamisi.
Mwanamama huyo alisimulia kuwa baada ya maneno kumfikia mke wa 
Jumanne, waligombana na mumewe ambaye alikasirika na kwenda kumpa kipigo
 kilichomsababishia maumivu makali kwa kuwa ni mjamzito.
“Alipomaliza kunipiga alikimbilia Kituo cha Polisi Mbagala, Dar wakaja kunikamata,” alisema kwa masikitiko.
Alidai kuwa polisi walipofika kumkamata walishangaa kumkuta katika maumivu makali kwani tumbo lilikuwa likimuuma kufuatia kiumbe kilichokuwa tumboni kukaa vibaya.
Alidai kuwa polisi walipofika kumkamata walishangaa kumkuta katika maumivu makali kwani tumbo lilikuwa likimuuma kufuatia kiumbe kilichokuwa tumboni kukaa vibaya.
PF3 aliyopatiwa Farida kutoka polisi baada ya kipigo cha Jumanne.
Alisema kuwa polisi waliwachukua wote huku wakimwamuru msanii huyo 
kutoa fedha za matibabu baada ya kupatiwa fomu ya matibabu (PF-3).
“Jumanne alinipa elfu 30, nikaenda kutibiwa Hospitali ya 
Mbagala-Zakhem ambapo waliniambia nimepata maumivu na mtoto amekaa 
vibaya,” alisema.
Farida alisema kuwa aliamua kumfungulia Jumanne kesi ambapo alipewa 
RB katika Kituo cha Polisi cha Mbagala, shitaka likiwa ni shambulio la 
kudhuru mwili hivyo msanii huyo anasubiri kufikishwa kwenye vyombo vya 
sheria.
Baada ya habari hizo kupenyezwa kwenye meza yetu, waandishi wetu 
waliwasiliana na Jumanne ambaye alikiri kuwa na matatizo kidogo ambayo 
walikwenda kuyamaliza kwa mkuu wa kituo.
-Gpl 
 
 
No comments:
Post a Comment