Muigizaji na mwimbaji nchini Kitale yuko Tanga alipoenda 
kuhudhuria Dua ya kumuombea marehemu Sharo Milionea ikiwa ni mwaka mmoja
 tangu afariki dunia kwa ajali mbaya ya gari.
Kitale ambaye ndiye msanii pekee aliyefika Tanga siku ya juzi amesema
 kuwa amejifunza mambo mengi katika msiba wa rafiki yake Sharo Milionea,
 ikiwa ni pamoja na misiba ya wasanii wengine waliotangulia mbele ya 
haki, Kanumba na Sajuki.
Akiongea kwa njia ya simu na Edson Mkisi katika kipindi cha Hatua 
Tatu cha 100.5 Times Fm, Kitale amesema kutokana na funzo alilopata 
ameampa ujumbe mama yake ili kwamba pindi atakapotangulia mbele ya haki 
mambo hayo yasijirudie kwake.
“Nimejifunza vitu vingi na nimejua marafiki walio wema na marafiki 
wasio wema. Ina maana kwamba kuna marafiki wanafiki na marafiki wasio 
wanafiki. Amesema Kitale.
“Kuna vitu vingi nimejifunza baada ya kuondoka marehemu Steven 
Kanumba, nimejifunza baada ya kifo cha Sharo Milionea, na nimejifunza 
baada ya kifo cha Sajuki. Nimejifunza vitu vingi sana sana sana.” 
Amesisitiza.
 “Ina maana hata mimi kama ntatangulia kuna mambo ambayo 
nimeshamweleza mama yangu na nimeshaieleza familia yangu, nafikiri 
hakitakuja kutokea kama kilichotokea kwa wenzangu. Nimejifunza vitu 
vingi hasa ukiwa msanii...” Kitale ameiambia Hatua Tatu.
Hata hivyo Kitale alikataa kueleza ujumbe huo na kudai kuwa ni siri 
kati yake na familia yake kwa kuwa hafahamu nani atatangulia kati yake 
na wazazi wake.
Kitale amewashauri wasanii kumkumbuka Mungu wakati wanapoendelea na 
shughuli zao na ndio sababu watu wengi wanaamini kuwa asilimia kubwa ya 
wasanii ni ‘Freemason’, na kwamba hiyo inatokana na kitendo cha wasanii 
hao kumsahamu Mungu wao.
Siku kama ya jana  mwaka uliopita (November 27,2012) ndio siku ambayo marehemu Sharo Milionea alizikwa huko Tanga.
 

 
No comments:
Post a Comment