Msajili wa Vyama vya Siasa,Jaji Francis Mutungi
Ofisi
 ya Msajili wa vyama vya siasa nchini, imethibitisha kupokea barua ya 
aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema ) 
mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Akizungumza
 na paparazi wetu kwa njia ya simu, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji 
Francis Mutungi, alithibitisha kupokea barua hiyo na kueleza kuwa ofisi 
yake inaifanyiakazi.
“Tumepokea barua ya Mwigamba, 
lakini siwezi kueleza kilichomo ndani yake kwa kuwa ndiyo tunaifanyia 
kazi…tutawaita wanahabari kuwaeleza hatua zilizochukuliwa na ofisi 
yangu,” alisema Jaji Mutungi.
Hivi karibuni katika mkutano 
na waandishi wa habari, Mwigamba ambaye amevuliwa madaraka yake yote 
ndani ya chama na wenzake, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na 
Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Kitila Mkumbo, aliwasilisha malalamiko yake 
kwa msajili.
Katika taarifa yake Mwigamba, 
amemuomba msajili kutoa mwongozo kuhusu anachodai kuwa ni mgogoro wa 
kikatiba uliopo ndani ya Chama kufuatia kipengele cha katiba 
kinachogusia ukomo wa uongozi kubadilishwa kinyume na utaratibu. 
“Katiba ya Chadema ya mwaka 
2004 kipengele 5.3.2 (c) inasomeka ifuatavyo kuhusu Muda wa 
Uongozi:Kiongozi aliyemaliza muda wa ungozi ana haki ya kugombea na 
kuchaguliwa tena mradi awe anatimiza masharti ya kuchaguliwa kuwa 
kiongozi kwa muda usiozidi vipindi viwili katika cheo kimoja kwa ngazi 
moja,” alidai Mwigamba.
“Sentensi kuhusu ukomo wa 
uongozi haipo. Ni kweli kuwa Marekebisho ya Katiba yalifanyika mwaka 
2006, lakini hoja ya kubadili kipengele hicho haikuwepo na muhtasari 
zinaonyesha wazi kuwa kulikuwa hakuna mjadala wa kipengele hicho au 
kuhusu suala zima la ukomo wa uongozi,” anadai. 
Novemba 22, mwaka huu, Kamati 
Kuu iliwavua madaraka viongozi hao na kuwataka wajieleze kwa maandishi 
ndani ya siku 14 baada ya kudaiwa kuhujumu chama kwa kuandika waraka wa 
siri unaodaiwa pamoja na mambo mengine, kuwadhalilisha viongozi wakuu wa
 Chadema.
 
 
No comments:
Post a Comment