
Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.
Kuna
 watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa 
uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.Mtu anaweza kuwa na mke 
na kujikuta kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna 
wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa 
mahari. Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa upande mwingine, lakini 
uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika kupoteza
 hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda ngono.
Pamoja
 na tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na 
kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema 
tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi cha kulazimika 
kufanya mapenzi kila tunapokutana hata kwenye nguzo ya umeme na chini ya
 miti kwa vile tu miili imetaka kufurahika.
 
Twende pamoja katika kutazama madhara hayo kwa kina.
KUPOTEZA HAMU YA TENDO.
Watu
 wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa 
wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza 
wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara.Sababu hizo zinaweza 
kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata 
anapomuona akiwa mtupu.
Aidha
 kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na 
kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu 
moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya
 mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu naye
 na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.
KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA.
Tabia
 ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini 
na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo 
la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa 
kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa 
wakati gani?
Watu
 wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao 
kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake.Hawa 
ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au 
kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa 
zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi.Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara 
kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku
 mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi.
KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO.
Raha
 ya tendo hutegemea sana hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na 
kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila 
mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha 
ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako.Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya
 kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!
KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI.
Madhara
 mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni 
pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili.Kama tujuavyo tendo la ndoa 
hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili 
uchoke. Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa 
nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha.Sambamba na hilo mbegu 
za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa 
dhaifu.
KUPATA MAGONJWA
.
Kama
 tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa
 na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia 
magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi, lakini ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na
 msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na 
kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko
 wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza 
kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi
 
 
No comments:
Post a Comment