Jana (November 21) B’Hitz Music Group iliweka wazi uamuzi wa
 kuwaondoa kwenye label hiyo wasanii watatu ambao ni Vanessa Mdee, 
Mabeste na Gosby.
Japokuwa Vanessa na Mabeste walitangaza wiki hii kujitoa kwenye label
 hiyo, huku Gosby akiwa bado hajasema chochote, timu ya BHits imesema 
kuwa wasanii hao waliondolewa kwenye label hiyo miezi miwili iliyopita 
japokuwa hawaamua kutangaza.
Mabeste aliiambia Times fm kuwa ameamua kujiondoa katika label hiyo 
kwa kuwa muziki wake ulikuwa haumlipi na kwamba maisha aliyokuwa anaishi
 ndiyo yaliyopelekea yeye kudhaniwa kuwa anafanya show za nje, na kwamba
 amechoka kuwa mzigo kwao.
Tovuti ya Times fm ilimtafuta Amani Joachim ambaye ni mwana sheria na
 Chief Operations Officer wa B’Hits Music Group ili kufahamu kuhusu 
sababu alizozitoa Mabeste kwa upande wa B’Hits, na mikataba ikoje na 
kama watachukua hatua zozote za kisheria.
“Hiyo statement ambayo Mabeste ameamua kuisema kwangu mimi naona 
haiko sawa kabisa. Sisi ni ndugu na tulikuwa tunaishi hivyo, tatizo la 
mtu mmoja ni tatizo la mtu mwingine yaani tunakuwa pamoja kabisa. Na 
kuna vitu vingi ambavyo Mabeste anajua kwamba tunavifumbia macho. Hata 
hiyo mikataba, sisi na Mabeste kuna kipindi tume-deal hata bila mikataba
 na mambo yakawa safi tu kwa sababu kuna ile heshima na kuaminiana.” 
Amesema Amani.
Ameyaelezea pia madai ya Mabeste kuwa mabadiliko yake katika maisha 
ndiyo yaliyosababisha B’Hits kuhisi kwamba anapiga shows za nje.
“Mabeste inabidi aangalie statements zake, na muda ambao anaamua 
kutoa hizo kauli kwa sababu kati yetu sisi tuna siri nyingi sana 
(Mabeste na Upande wa B’Hits). Tusifike sehemu kwamba tukaanza 
kufaidisha kila mtu, hicho ndicho kitu ambacho ningependa kukiweka sawa.
 Hizo shows na vitu vingine ambavyo labda alikuwa anavifanya akiwa nje 
tunavifahamu vingi tu, lakini kutokana na ule u-brother na nini 
tunavichunia tu.” Ameeleza kiongozi huyo wa B Hits.
Hata hivyo Amani amekubaliana na kuwepo kwa ubovu wa soko la muziki 
ambapo amesema hata shows zikiwepo bado malipo yanayotolewa yako chini 
kiasi kwamba Kampuni haliwezi kuendeshwa kwa kutegemea kugawana kipato 
hicho na msanii.
Aliongelea pia madai ya Mabeste kuwa B’Hits haikuwa inamfanya atengeneze pesa kupitia muziki wake.
“Well, hopefully kule anakoenda atapata. Tunaelewa Mabeste ana 
majukumu, maisha yake tunajua kwamba yamebadilika kwa namna flani. 
Personally nafahamu, sijui akina Harmy na Pancho. That’s why I’m ready 
to stay quiet kwenye vitu kama hivyo, nilikuwa tayari kukaa kimya…sina 
haja ya kufunguka ni vitu vingapi ambavyo Mabeste ameshafanyiwa katika 
hali ya u-brother, I will not say them kwa sababu kipindi mimi navifanya
 nilivifanya katika good will na nilitaka iishie hivyo, Amani will never
 say them.”
C.E.O wa B'Hits Hermy B aliuambia mtandao wa Bongo5 kuwa Vanessa, 
Gosby na Mabeste hawana shukurani kwa kile ambacho B Hits imewafanyia na
 kutoa mfano kuwa alitoa shilingi million nane mfukoni kulipia video ya 
Closer ya Vanessa  na kiasi kingine kulipia kazi alizofanya nje ya 
studio za B Hits, fedha ambazo hazijawahi kurudi.
Nae Amani Joachim alitoa ushauri kwa Vanessa, Mabeste na Gosby kwa 
ujumla kuwa wawe na amani na waendelee kufanya mambo yao na kuacha 
kutengeneza vita kati yao na B’Hits kupitia media kwa kuwa hata yeye 
ameamua kuyafumbia macho mengi.  
Lakini vipi kuhusu hasara ambayo B’Hits itaipata kutokana na kuondoka
 kwa wasanii hao kwa kuwa walichukuliwa wakiwa hawana majina na wakati 
huu wanaondoka wakati wameanza kuwa productive.
Mwana sheria na Chief Operations Officer wa B’Hits anaeleza.
“They were real productive na naweza kukwambia kweli hawa watu wako 
very talented, na B’Hits haijawahi kum-house mtu ambaye ni mbovu, na ndo
 maana watu wanashangaa kwa nini mna nyumba kubwa ya media halafu mna 
watu watatu tu, sisi kuna kipindi tulikuwa na msanii mmoja tu Mabeste 
for like 4 years, ni kwa sababu tunaangalia talent.
“Na kusema kwamba sasa hivi tutakuwa hatujarudi nyuma utakuwa ni 
uongo, kuondoka kwao ndio tutarudi nyuma steps kadhaa, lakini pia 
kutokana kwamba plans tulizopanga kufanya wakati tukiwa nao zilikuwa 
hazijafika kuiva, we are ready to do that with someone else, Mungu 
hajagawa kipaji kwa watu wawili au watatu.”
Amesema anaamini baada ya Gosby, Vanessa, na Mabeste watakuja watu wengine ambao wana vipaji pia.
Kauli ambayo inaungana na ile ya Hermy B kuwa B’Hits itatangaza wasanii wapya wa label hiyo mwanzoni mwa mwaka ujao.
Tovuti ya Times fm ilitaka kufahamu kutoka kwa mwana sheria huyo 
kuhusu mkataba kati ya B’Hitz na wasanii hao na damages/athari za 
kuvunja mkataba huo zikoje na iwapo watawadai wasanii hao.
Amesema mikataba ilikuwa tight lakini kwa mazingira ya Tanzania na 
hali halisi ya kipato cha wasanii wa Tanzania hiyo mikataba inakuwa kama
 useless kwa kuwa kiasi kinachotakiwa kulipwa na msanii huyo ni kikubwa 
kuliko hali halisi ya maisha ya msanii husika.
“Ukimchukua bwana mti ukampeleka mahakamani, mahakama inaangalia 
damage ambayo imeingia katika kampuni, na mwisho wa siku inachukua 
maamuzi ambapo itakwambia bwana mti kama amepatikana na kosa amlipe 
bwana jose million 150 Kwa mfano, haimfungi. Problem ni kwamba bwana mti
 hana hata shilling 200 mfukoni mwake, we unadhani utamfanyaje bwana 
mti?” Alieleza kwa mfano.
“Kwa sababu mahakama ikishakupa judgement inakuacha ukatafute hiyo 
hela, haimfungi mtu. Kesi za madai sio kesi za jinai..sasa hapo imagine 
hapo ni wasanii wangapi leo unawafanyia kazi ya million 40 Million 50, 
ambayo ukiingia katika intellectual property court (mahakama ya maswala 
ya copy right), na copy right ni very expensive, tunaongelea six 
figures, eight figures. Sasa angalia ni wasanii wangapi hapa Tanzania 
wanaweza kukulipa eight figures.?” Amesema.
Kutokana na hali hiyo amesisitiza kuwa kuna haja ya kuwalipa wasanii 
pesa nyingi katika kazi zao huko wanakoenda kufanya ili wanapopata 
matatizo waweze kulipa, na kwamba bila hivyo mikataba ya label na 
wasanii Tanzania itakuwa useless.
Hii inamaanisha kuwa hakuna hatua zozote za kisheria ambazo B’hits itachukua kudai fidia kutoka kwa wasanii hao.
Hata hivyo uongozi wa B’Hits umesema utaachia nyimbo nyingine za 
wasanii hao zilizoko studio na kwamba zitachezwa redioni, lakini wasanii
 hao hawatakuwa na haki ya kuzitumia kwa kuwa ni mali halali ya kampuni 
hiyo.
Msikilize hapa Amani Joachim:
 
 
No comments:
Post a Comment