Katika
 kuelekea ufunguzi wa mgahawa wao magwiji wa soka wa klabu ya Manchester
 United Ryan Giggs na Gary Neville jana waliingia kwenye mashindano ya 
kupika misosi.
Giggs
 na Neville kwa pamoja jana walishiriki kwenye mashindano hayo 
yaliyofanyika maeneo ya Westfield Stratford City shopping centre jijini 
London ikiwa ni moja ya shamrashamra ya ufunguzi wa mgawaha wao wa Cafe 
Football.
Wawili hao walishindana na mpishi mkuu wa mgahawa huo, Brendan Fyldes pamoja na mpishi wa Michelin chef Michael Wignall.
Giggs
 na mwenzie walipika vyakula vikuu vitatu ambavyo vitakavyokuwa 
vikipatikana hapo vikiwemo Nev's Noodle Pot, Wignall's Halftime Orange 
na Chocolate Pistachio Turf.
Neville
 alisema: 'Shindano hili lilikuwa nafasi nzuri kwa wanunuzi Westfield 
Stratford City kuona nini tumewaandalia kwenye Cafe Football.
'Mapishi matatu tuliyopika ni mfano tu uzuri wa vyakula ambavyo vitakuwa vikipatikana Cafe Football.
Mgahawa huo utafunguliwa rasmi mwezi ujao. 
 
 
No comments:
Post a Comment