adsence

Pages

Wednesday, November 27, 2013

MSANII HUYU WA BONGO MOVIE AAMINI NDOA NI CHUO CHA MAFUNZO BAADA YA KUOLEWA..!!


MSANII wa filamu za Kibongo, Halima Yahya ‘Davina’ amekiri kujifunza mambo mengi ya maisha baada ya kuingia kwenye ndoa.
Halima Yahya ‘Davina’.
Akizungumza na mwandishi wetu, Davina alisema kwamba anaichukulia ndoa yake kama chuo cha mafunzo kwa jinsi alivyobadilika na kuwa tofauti na Davina aliyekuwa nje ya ndoa.
“Nimekuwa tofauti kabisa na Davina wa kabla ya ndoa, sasa hivi kila kitu nakifanya kwa ustaarabu kwa kuwa najiona nimekuwa mwenye majukumu

mengi,” alisema.
Akifafanua zaidi, Davina alisema zamani alikuwa ni mtu wa kurandaranda hovyo tofauti kabisa na hivi sasa.
“Zamani nilikuwa napenda safari zisizokuwa na faida tofauti na sasa hivi, kweli nimeamini ndoa ni chuo cha mafunzo,” alisema huku akiwaombea wasanii wenzake walio nje ya ndoa wafunge ndoa na kuwa na familia zao kwani watajifunza mengi.


-GPL

1 comment:

  1. NoVCasino Casino - NOVCASINO.COM
    NoVCasino.com offers https://vannienailor4166blog.blogspot.com/ a no deposit bonus poormansguidetocasinogambling of 100% up to €150. febcasino.com No Deposit Bonus kadangpintar is given novcasino to new players only. No deposit bonuses expire

    ReplyDelete