adsence

Pages

Wednesday, December 4, 2013

HILI NI BALAA tena kwa RAGE Simba.....SOMA ZAIDI HAPA

 Mwenyekiti wa Simba aliyesimamishwa, Ismail Aden Rage.
  
MWENYEKITI wa Simba aliyesimamishwa, Ismail Aden Rage, amepingwa kwa mara nyingine na wajumbe wa kamati ya utendaji ya timu hiyo, kufuatia maamuzi ya kuwateua Michael Wambura na Rahma Al Kharusi, maarufu kama Malkia wa Nyuki.

Akizungumza na mwandishi wetu, Swedi Nkwabi ambaye ni Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, alisema Rage katika kuwateua Wambura na Malkia wa Nyuki ni hatua nyingine ya kiongozi huyo kuvunja katiba ya klabu hiyo.
 
“Katiba ibara ya 28 kipengele D, inatamka wazi kuwa mwenyekiti amepewa nafasi ya kuteua wajumbe wawili, ambao kati ya hao tayari Rage alishamteua Zacharia Hans Pope kuwa mjumbe wa heshima, huku akibakiza nafasi moja ambayo bado haijakamilishwa vigezo vyake.
 
“Siku zote tunasema Rage anavunja katiba, watu huwa hawatuelewi,” alisema Nkwabi huku akiongeza kwa kusema:
 
“Nafasi moja iliyosalia Rage kama angekuwa madarakani, angeweza kuitumia lakini ni mpaka pale ambapo angeunda kwanza baraza la wazee ambalo wakati  tunamsimamisha hakuwa ameliunda.
 
“Baraza la wazee linaundwa na wajumbe wanne wa wadhamini wa klabu, wajumbe wanne kutoka baraza la walezi wa klabu na wajumbe watano ambao hawa wanachaguliwa katika kikao cha wadhamini na walezi, kikao ambacho mpaka tunamsimamisha alikuwa hajakifanya.

“Lakini pia angalia amemteua Malkia wa Nyuki kuwa mjumbe wa baraza la wadhamini wakati tayari kolamu yao imeshatimia baada ya kumteua Patel (Ramesh), Mzee Kilomoni (Hamis), Samuel Sitta na Aluu Habu ambapo sasa kama amemteua na Malkia wa Nyuki watakuwa watano.”
 
Aidha, Nkwabi amesema kamati yake haina tatizo na Wambura au Malkia wa Nyuki ambao wote bado michango yao inahitajika ndani ya Simba lakini tatizo kubwa lipo kwa Rage ambaye amewaingiza bila kufuata taratibu.
credit: champion via gpl

No comments:

Post a Comment