Kwa
 mujibu wa jarida  Bloomberg BusinessWeek, Bieber aliifuata kampuni hiyo
 mwaka 2007 (kipindi ambacho hakuwa maarufu) na kuwaomba awe balozi wao 
(brand ambassador).
Aliyekuwa Meneja Mkuu wa maendeleo ya biashara wa RIM alisimulia:
“Kitu
 kimoja tulichokikosa kilikuwa kwamba Justin Bieber alitaka kuwa 
mwakilishi wa BlackBerry. Alisema:  Nipeni $200,000 na simu 20 na 
ntakuwa balozi wenu. Tuliwapelekea wazo watu wa masoko na kuwaambia:  
Huyu ni mtoto wa Canada, alikulia hapa, watoto watapenda.  
Walitufukuza
 na kusema ‘huyu mtoto ni wa muda. Hawezi kufika popote. Na mimi kwenye 
mkutano niliwaambia ‘huyu mtoto atadumu zaidi ya RIM.” Kila mmoja 
alicheka.
Of course, mwaka 2013 RIM walibadili jina na kuwa BlackBerry. Bieber … bado anaitwa Bieber.
Kipindi
 hicho kampuni ilikuwa hata haifanyi matangazo kwakuwa umaarufu wake 
kwenye biashara uliwapa kiburi kuwa watu wangenunua tu simu. Mambo 
yalianza kuwa magumu kwa Blackberry baada ya simu iPhone na zinazotumia 
mfumo wa Android kushika kasi.
Mwaka
 huu pekee, kampuni ya Blackberry imepoteza dola bilioni 1 kwa miezi 
mitatu pekee.  Kwa miaka mitano iliyopita, thamani ya kampuni hiyo 
imeshuka kwa asilimia 85 hadi kufikia dola bilioni 4  kutoka dola 
bilioni 80 mwaka 2008.
Mwaka
 2013, kampuni ya Fairfax ilitoa ofa ya kuinunua BlackBerry kwa dola 
bilioni 4.7. Mwezi  September, kampuni ilitangaza kuwaachisha kazi 
wafanyakazi 4,500.
Wakati
 huo huo, Justin Bieber ameendelea kupeta. Kwa sasa ana utajiri wa 
$130million,na amekamata nafasi ya 9 ya Forbes ya mastaa wenye ushawishi
 zaidi duniani.
Pole yao Blackberry.
 
 
No comments:
Post a Comment