Bomu limeokotwa karibu na eneo la Kanisa la Huduma ya Maombezi ambalo 
pia ni eneo la makazi ya watu katika barabara ya Barakuda Kata ya 
Mazimbu Manispaa ya Morogoro.
Bomu hilo liliokotwa juzi  asubuhi na mtoto ambaye alikuwa akilima 
bustani jirani na nyumba yao  na baada kuchimbua udongo aliona kitu 
kizito na kukitoa.
Mmoja mashuuda, Brayton Sospeter, alisema bomu hilo liliokotwa na mtoto 
huyo na baadaye kulichukua na kwenda kuwaonyesha watoto wenzake 
waliokuwa wakicheza katika eneo hilo.
Alisema watoto hao waliendelea kulichezea 
na baadaye kumuonyesha mzee mmoja liyekuwa akipita katika eneo hilo na kugundua kuwa ni bomu, hivyo kutoa taarifa Polisi.
Sospeter alisema baadaye  Polisi walifika katika eneo hilo na 
kuthibitisha kuwa ni bomu na kueleza kuwa ni kubwa hivyo hawana uwezo wa
 kulitoa katika eneo hilo na badala yake walizungushia uzio huku 
wakiahidi kwenda kuwasilina na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa 
ajili ya kulitoa katika eneo hilo.Hata hivyo wanajeshi hawakufika.
Naye mmoja wa waumini wa kanisa hilo, alijitambulisha kwa jina la mama 
Maloda, alilalamikia vyombo vya usalama kutoliondoa licya ya 
kuthibitisha kuwa ni bomu.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, John Laswai, alithibitisha 
kuwepo kwa taarifa hizo na kwamba walikuwa wakiwasilina na JWTZ ili 
kwenda kulitambua.
Hadi jana mchana, bomu hilo liliendelea kuwapo eneo hilo bila JWTZ kufika.
CHANZO: NIPASHE
 
 
No comments:
Post a Comment