Huenda
 ukawa umejiuliza swali hili kwa kipindi kirefu lakini hujawahi kupata 
jibu. Kwanini Tanzania, Afrika Kusini na Zambia zinatumia wimbo wa taifa
 wenye melody inayofanana?
Enoch Sontonga
Wimbo
 huo ulianza kutumika kama wimbo maalum wa hekaheka za ukombozi wa 
Afrika na baadaye kuanza kutumiwa kama nyimbo za taifa za nchi tano 
barani Afrika, zikiwemo Zambia, Tanzania, Namibia na Zimbabwe baada ya 
kupata uhuru.
Zimbabwe
 na Namibia zimepata nyimbo zingine za taifa. Wimbo huo kwa sasa 
unatumika Tanzania, Zambia na tangu mwaka 1994 kama sehemu ya wimbo wa 
taifa wa Afrika Kusini.
Hata
 hivyo ikumbukwe kuwa Tanzania ndio ilikuwa nchi ya kwanza kuanza 
kuutumia wimbo huo kama wimbo wa taifa 1961 pale ilipokuwa Tanganyika na
 kuendelea nao baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964
Tafsiri ya mashairi ya awali yaliyokuwa kwa lugha Xhosa kwenda Kiswahili ilifanya na kundi la watu.
Wimbo
 unaotumiwa na Afrika Kusini hata hivyo ni mchanganyiko wa “Nkosi 
Sikelel’ iAfrika” na “The Call of South Africa” (unaojulikana kwa lugha 
ya Afrikaan kama “Die Stem van Suid Afrika”).
20
 April, 1994 ndipo ilipotangazwa kwamba zote Nkosi Sikelel’ iAfrika na 
Die Stem ziwe nyimbo za taifa za Afrika Kusini. Wimbo uliounganishwa 
ulianza kufanya kazi October, 1997, baada ya maneno ya Kiingereza 
yalipoongezwa na wimbo kupangwa upya na Jeanne Rudolph.
 


 
No comments:
Post a Comment