TP 
Mazembe tayati imetua mjini Tunis, Tunisia kwa ajili ya Fainali ya 
kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji Sfaxien kesho 
ikiwa na washambuliaji wawili wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally 
Samatta na Thomas Emanuel Ulimwengu. Ulimwengu na Samatta waliicheza 
Tanzania, Taifa Stars Jumanne mchezo wa kirafiki dhidi ya Zimbabwe 
ulioisha kwa sare ya bila kufungana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na 
baada ya mechi wakaenda kuungana na klabu yao iliyokuwa kambini 
GhanaBaada ya wiki moja ya kambi yake Lizzy Sports Complex mjini Accra, 
Mazembe iliondoka Jumatano asubuhi na kutua jioni Tunis. Baada ya safari
 ya saa nne (4) na dakika 45 kwenye ndege, waliwasili Uwanja wa ndege wa
 Carthage mjini Tuni
Baada ya 
kuwasili, Robert Kidiaba na Cheibane Traore pamoja na kocha Patrice 
Carteron walijibu maswali ya Waandishi wa Habari wa Tunisia kabla ya 
timu kwenda kupumzika hotelini kwa dakika 30 kisha kwenda kufanya 
mazoezi.
Sfaxien, 
timu pekee iliyoshinda Kombe la Shirikisho mara mbili tangu 
kutambulishwa kwa mfumo mpya mwaka 2004, maskani yake ipo katika mji 
uliozungukwa na bahari ya Mediterranean, Sfax.
Mechi ya 
marudiano itachezwa mjini Lubumbashi, DRC Jumamosi ijayo, ya Novemba 30 
na mshindi atajinyakulia kitita cha dola za Kimarekani, 625 000 wakati 
mshindi wa pili atapata dola 432 000.
Mshindi 
pia atamenyana na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ya Misri kuwania
 taji la Super Cup mechi itakayopigwa nchini Misri Februari 2014. 
Chanzo: binzubeiry
 
 
No comments:
Post a Comment