MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Rutamba, Wilaya ya Lindi 
amekutwa akiwa na nguo za ndani pekee katika usingizi mzito kwenye kibao
 cha shule hiyo huku akiwa hajitambui kwa madai ya kilichomkutana 
kinahusishwa na imani za kishirikina.
Tukio hilo limetokea juzi usiku baada ya mkazi 
mmoja wa kijiji hicho, Juma Mbilemoto kumkuta mwalimu huyo akiwa kwenye 
kibao hicho wakati alipokuwa anamsindikiza nduguye,Aisha Mbilimoto 
aliyekuwa anasafiri kuelekea Dar es Salaam.
Akizungumzia tukio hilo, shuhuda huyo alisema 
alimkuta mwalimu huyo akiwa amelala chini ya kibao cha shule akiwa na 
nguo ya ndani tu (chupi)huku akikoroma kutokana na kuwa na usingizi 
mzito.
Alisema awali hakumtambua mtu huyo lakini baada ya kumkaribia alimtambua kuwa alikuwa mwalimu mkuu wa shule hiyo na ndipo alipochukua jukumu la kumwamsha ili amvalishe kanga, lakini aliikataa na kuondoka kwenda nyumbani kwake akiwa kama alivyokutwa
Alisema awali hakumtambua mtu huyo lakini baada ya kumkaribia alimtambua kuwa alikuwa mwalimu mkuu wa shule hiyo na ndipo alipochukua jukumu la kumwamsha ili amvalishe kanga, lakini aliikataa na kuondoka kwenda nyumbani kwake akiwa kama alivyokutwa
Kwa upande wao walimu wa shule hiyo walisema kuwa,
 wamekosa molari wa kufanya kazi kutokana  na kitendo alichofanyiwa 
mwalimu mwenzao.
Akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake mwalimu wa
 taaluma wa shule hiyo, Francis Milanzi alisema  walimu shuleni hapo 
wamekosa amani na kuwasababishia kuzihama nyumba zao  kwa muda na badala
 yake kwenda kukesha  kwenye ofisi za walimu tangu tukio hilo litokee.
Ofisa elimu wa Wilaya ya Lindi, Cosmas Magigi 
alisema amepokea taarifa za tukio hilo kwa huzuni na amewaomba walimu 
kuwa na subira wakati utaratibu wanalishughulikia suala hilo.
Magigi aliongeza kuwa ofisi yake itafanya 
utaratibu wa kumhamisha  mwalimu huyo na kumtafutia shule nyingine huku 
akiwataka wakazi wa eneo hilo kujenga ushirikiano na watumishi ili 
waweze kutekeleza majukumu yao.
CHANZO: MWANANCH
 
 
No comments:
Post a Comment